Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

MPANGAJI DAR ATOA KERO ZAKE JUU YA WENYE NYUMBA

Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.
Leo katika kipindi cha Kero Yangu tuna angazia kwenye swala la wenye nyumba na wapangaji katika eneo la Mbagala Kipati mtaa wa Mangaya jiji la Dar es salaam.

Kiukweli kabisa wapangaji wamekuwa ni watu wenye kunyanyaswa sana na wamiriki wa nyumba, nyie wenye nyumba ebu kuweni na moyo wa uruma kwa wapangaji wenu jamani.
Maana vitendo mnavyo wafanyia wapangaji wa nyumba zenu havifai katika maisha ya leo, utakuta wapangaji mnachanga pesa ya kununua umeme kisha mkisha uweka umeme yatari mama/baba mwenye nyumba anatumia umeme huo kinyume na makubariano yenu.

Mfano wa matumizi ya umeme kinyume na makubariano ni kama kupasha maji moto au kupika chai kwa kutumia jiko la umeme, kuwasha fridge, kupiga pasi mda wote nk.

Mbali na hayo kuna baadhi ya wapangaji hushindwa kukaa kwenye baadhi ya nyumba kutokana na masharti ya nyumba hiyo kuwa magumu kupita maelezo, mfano wa masharti hayo yaweza kuwa ni kukatazwa kupika chakula kizuri kuliko mwenye nyumba, nk.

Ila ukiachilia matukio kama hayo, bado kuna tatizo la madarari kupandisha bei ya nyumba/vyumba ili waweze kupata malipo makubwa, bado tukumbuke ya kwamba mbali na wapangaji kutozwa kodi kubwa serikali hainufaiki na chochote kutoka kwa wapangaji mbali ya malipo ya ardhi kwa zile nyumba zilizo kwenye maeneo yaliyo pimwa.
Mkataba wa pango la nyumba ninayopanga unasema umeme ni Tsh 10,000 tu kwa mwezi, ila baada ya kuja mke wa mtoto wa mwenye nyumba matumizi yamekuwa makubwa kupita kiasi, pindi akisafiri waga umeme wa Tsh 10,000 unakaa zaidi ya siku 10, ila akirudi umeme wa pesa hiyoiyo 10,000 ni siku 4 tu.

Na hii ndio ilikuwa kero yangu, naitwa Zaituni Hally, kutoka Mbagala Kipati mtaa wa Mangaya. Wenye nyumba mbadilike maana sisi ndio tunao waweka mjini, mnatakiwa kutuheshimu na kusikiliza mawazo yetu maana hata sisi tuna aki ya kusikilizwa pia kama binadamu wengine.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.

Share habari hii na wenzio wajue

Post a Comment

CodeNirvana
Powered by Blogger.
© Copyright Tazama Line
Back To Top