Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

TANZANIA YA ADHIMISHA SIKU YA HEDHI DUNIANI

Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.
Tanzania imeadhimisha siku ya hedhi duniani, ambapo wizara ya elimu kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wamekubaliana kuandaa na kusimamia sera inayoondoa vikwazo kwa watoto wa kike katika masomo yao.

Akizungumza katika maadhimisho hayo jana jijini Dar es Salaam, Ofisa Elimu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Madina Kemilembe, alisema kukosekana kwa miundombinu rafiki mashuleni kunasababisha wanafunzi kutohudhuria masomo.

Alisema ukosefu wa mazingira bora kama vyoo, maji safi na salama pamoja na vyumba mahsusi vya kubadilishia nguo , hasa kwa watoto wa kike wanapokua katika hedhi mashuleni kunachangia utoro.
“Nawashukuru wadau Water Aid, Shirika la Maendeleo la Uholanzi (SNV), Kasole Secrets pamoja na wengine kwa kuisaidia serikali kuandaa mazingira rafiki kwa watoto wetu kwa kuwajengea vyumba vya kubadilishia na kuhakikisha upatikanaji wa pedi kwa baadhi ya shule,” alisema Kemilembe.

Alisisitiza juu ya utoaji wa elimu kwa wazazi na wanafunzi wa jinsia zote ili kuondoa unyanyapaa ili kuboresha mazingira ya kusoma kwa mtoto wa kike. Naye Mkurugenzi wa Water Aid, Ibrahim Kabole, alisema kuna uelewa mdogo pamoja na mila potofu zinazofanya jambo la hedhi kuonekana ni la aibu.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.

Share habari hii na wenzio wajue

Post a Comment

CodeNirvana
Powered by Blogger.
© Copyright Tazama Line
Back To Top