Mimi chakuwashauli vijana wote wakiume nikwamba pindi wewe kijana wakiume ukijisikia kabisa kwa moyo wako mkunjufu kuwa unataka kuwa na msaidizi wako wa maisha yako yote. (Mkeo awe ni wa ndoa ya kanisani au msiktini au ndoa zetu zile bubu)
Ni vyema ukubali kutumia mda wako mwingi kutafuta yule unayeona anavigezo vyote na asiwe wa kutaftiwa umtafute wewe mwenyewe ili kuondoa ugomvi wa hapo baadae wa wewe kumwambia ukumchagua, na kutokea hapo nadhani utampenda kwa moyo wako wote na utamuweka wazi kwa kila jambo maana tayari na yeye atakuwa anajua malengo yako kwake.
Lakini na kwa upande wa akina dada nanyie pindi ukimpata mtu ambaye amekutamkia kuwa anakupenda na akaweka wazi mipango yake juu yako ni vyema ukamsapoti kwa moyo mmoja kuliko kuanza kumdisappoint sawa!?.
Maana asilimia kubwa ya wasichana wakisha ambiwa na mwanaume kuwa anataka amuoe waga wana anza kulinga wakimaanisha kuwa kitendo cha kuambiwa kuolewa basi wao wanathamani kubwa sana kuliko wale ambao hawaja ambiwa vile.
Kumbuka kitendo cha kuanza kumlingia yule bwana na kumuonesha vitabia vya ajabu ambavyo hakuwai kuviona kwako tayari unakuwa umepoteza 40% ya uhaminifu kwa yule mtu ndani ya kipindi cha uchumba wenu. (Tabia hii sio kwa wadada tu bali hata pia kwa wanaume).
Swali ni je iyo asilimia 60 iliyobaki itatosha kuendesha maisha ya ndoa yenu? au ndo mnataka ndoa yenu iwe kana ya akinafulani inafungwa asubuhi na ikifika jioni inavunjwa?
Kwaiyo ni vyema kila mmoja akaweka wazi malengo na mikakati yake kwa mwenzi wake.
Naitwa Mutalemwa, kwa maswali, maoni au ushauri napatikana kupitia simu namba 0659 919292 endelea kuwa nasi tukujuze zaidi kupitia Mutalemwa Blog >>
Post a Comment