Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

ARSENAL NA MAN UNITED KUMBE NGUVU SAWA?

Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.

wameshikilia nafasi yao ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England (EPL) baada ya kutoka sare ya 1-1 na Manchester United.
Sare hiyo imewaacha United wakiwa nafasi ya nne, ambapo bao lao lilifungwa na Andre Herrera wakati la Arsenal lilisababishwa na majalo ya Theo Walcott iliyomparaza Blackett.

Ilikuwa mechi ambayo kipa namba moja wa United, David de Gea alilazimika kuondoka uwanjani baada ya kuumia na kwa mara ya kwanza Victor Valdes kuchukua nafasi yake katika EPL.

Arsenal watajihakikishia nafasi ya tatu iwapo watawafunga Sunderland Jumatano hii. Timu zote mbili zimejihakikishia nafasi kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL) japokuwa kinachogombewa ni nafasi ya pili, tatu na ya nne.

Tayari Chelsea wametwaa ubingwa, hivyo nafasi tatu zinazofuata zinawaniwa na Manchester City, Arsenal na Man United.

Katika mechi nyingine, Man City wamewafunga Swansea 4-2 katika mechi iliyoshuhudia mchezaji wa zamani wa Swansea, Wilfried Bony akifunga bao la mwisho na kuwaadhibu klabu yake ya zamani.

Mabingwa hawa waliovuliwa taji na Chelsea majuzi walicheza vyema, ambapo mabao yao mengine yalifungwa na Yaya Toure mawili na jingine James Milner, wote wakitarajiwa kuondoka klabuni hapo msimu huu.

Swansea walipata mabao yao kupitia kwa Gylfi Sigurdsson na Bafetimbi Gomis, wakiweka rehani matumaini ya kupata kucheza Ligi ya Europa kwani sasa wanashika nafasi ya nane wakiwa na pointi 56.

Chelsea ambao ni mabingwa wanaongoza ligi wakiwa na pointi 84 wakifuatiwa na Man City wenye pointi 76, Arsenal wanazo 71 lakini wana mchezo mmoja mkononi kama walivyo Sunderland.

Nafasi ya nne wanashika United wakiwa na pointi 69, wa tano ni Liverpool wenye pointi 62 wakifuatiwa na Southampton wenye pointi 60.
Mkiani bado wapo QPR wenye pointi 30 sawa na Burnley huku Hull wakiwa nazo 36 na Sunderland waliojikusanyia pointi 37.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.

Share habari hii na wenzio wajue

Post a Comment

CodeNirvana
Powered by Blogger.
© Copyright Tazama Line
Back To Top