Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

KERO YANGU NDANI YA KILWA ROAD DSM

Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.
Ndugu mdau karibu sana kwenye ukurasa mpya kabisa unaoitwa Kero Yangu. Ukurasa  huu utakuwa ukichapishwa kupitia Mutalemwa Blog live kutoka Dar pamoja na Tazama line.
Lengo la ukurasa  huu nikutazama pale palipo sahaulika na kuwakumbusha wahusika ili wakapafanyie kazi. Pia ukurasa huu hauishii hapa Dar es salaam tu, bali mpaka mikoani.

kwaiyo kama kuna jambo ambalo halijawekwa sawa na wahusika iwe ni Serikali,  watu binafsi au taasisi mbalimbali waweza kuwasilisha kero yako na sisi tutaichapisha mtandaoni ili iweze kupatiwa ufumbuzi wakudumu kutoka kwa mlengwa/walengwa/muhusika/wahusika.

Kwakuanza leo tuanzie kwenye barabara ya Kilwa (kilwa road), katika barabara hii kumekuwa na maoni tofauti juu ya watumiaji wakuu wa barabara hii ambao ni wakazi wa Temeke, Tandika, kwa Azizi Alli, Mtoni mtongani, Mission,  Mbagala kuu, Mbagala rangi tatu,  na maeneo mengine yaliyoko kwenye ukanda wa mwambao wa kusini.

Kuna kipande korofi sana ambacho kimeanzia eneo la sabasaba maonyesho mpaka Mtoni Mtogani. Kiukweli kipande hiki kina watesa sana watumiaji wa barabara hii,  maana wanasema kwamba tangu kipande hicho kilipo kwanguliwa mwaka jana kwa ajili ya kufanyiwa marekebisho mpaka sasa bado hakuna kilicho fanyika zaidi ya wakazi wa maeneo hayo kuoga vumbi wakati wa kiangazi huku magari yakiaribika nyakati za mvua kutokana na mashimo makubwa yaliyoko kwenye eneo hilo.

Kwaiyo jamani naomba kuungana na wananchi wote wanao tegemea barabara hii kama mkombozi wao tunaomba mamraka husika muweze kutatua kero hii kwa watumiaji wa barabara hii ya Kilwa maana ina wakwamisha katika mambo yao, mfano kuchelewa kazini nk.
Kwa maoni/ushauri au kero yako basi waweza kutuma ujumbe wako kwa sms au what's up  kupitia 0659919292 kumbuka kutaja majina yako kamili na sehemu ulipo kisha ujumbe wako tutauchapisha na utawafikia wahusika. 
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.

Share habari hii na wenzio wajue

Post a Comment

CodeNirvana
Powered by Blogger.
© Copyright Tazama Line
Back To Top