Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

UNAJUA MADHARA YA KUVUTA SIGARA WAKATI UKIWA MJAMZITO?

Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.
Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha tofauti kubwa katika idadi ya wanawake wanaovuta sigara wakiwa na mimba nchini Uingereza, maeneo maskini yakiwa na idadi ya juu.

Takwimu hizo zinaonyesha 20.2% ya wajawazito eneo la Blackpool huvuta sigara katika kipindi cha ujauzito wao ikilinganishwa na 2.1 eneo la matajiri la Westminister.

Kila mwaka zaidi ya mimba 70,000 huathiriwa na uvutaji wa sigara.
Kwa jumla kiwango cha kadiri cha uvutaji sigara kimepungua chini ya asilimia 11 nchini Uingereza lakini ripoti ya shirika la Smoking in Pregnancy Challenge inapendekeza viwango hizo chini ya asilimia sita ifikapo 2020.


Profesa Russel Viner wa chuo cha udaktari cha watoto kiitwacho Royal Colledge Child Health amesema viwango vya uvutaji sigara miongoni mwa wanawake wachanga wenye mimba imo juu zaidi

"Wana uwezekano mara sita zaidi wa kuvuta sigara wakiwa waja wazito wakilinganishwa na wanawake waliopitisha umri wa miaka 35.”

"Pia tunajua kuna tofauti kubwa ya kikanda na viwango vya juu zaidi vimo katika jamii fukara. Tunafaa kuchukulia suala hili kwa uzito."

Daktari wa uzazi wa chuo cha Royal College of Obstetricians David Richmond amesema ni muhimu sana kwa wanawake wajawazito kuacha kuvuta sigara wanaposhika mimba.

”Hili husaidia kuboresha afya ya mtoto, kukua kwa mtoto huyo na pia kupunguza matatizo ya ujauzito yanayoweza kuepukika," amesema.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.

Share habari hii na wenzio wajue

Post a Comment

CodeNirvana
Powered by Blogger.
© Copyright Tazama Line
Back To Top