Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

UKOSEFU WA MADAWATI WASABABISHA WANAFUNZI KUSOMEA NJE WAKIWA WAMEKAA CHINI, BOFYA HAPA KUJUA ZAIDI

Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.

Ukosefu wa madawati wasababisha wanafunzi kusomea nje wakiwa wamekaa chini.

Wanafunzi wa shule ya msingi Simanjiro kata ya Emboreti mkaoni Manyara wanalazimika kusomea nje wakiwa wamekaa chini kwenye vumbi,na wengine kubanana kwenye madawati chakavu  kutokana na shule hiyo kukabiliwa na ukosefu wa madawati,na vyumba vya madarasa.

Mkuu wa shule hiyo mwalimu Lightness Lukumai amesema madawati yaliyopo shuleni hapo ni chakavu ambayo hayatoshelezi idadi ya wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo hali ambayo inawafanya walimu wachache waliopo katika shule hiyo kufanyakazi katika mazingira magumu.

Amesema muamko wa wananchi wa jamii ya kimasai kusomesha watoto kwa sasa ni mkubwa ikilinganishwa na miaka ya  nyuma na kwamba changamoto kubwa ni utoro unaosababishwa na wanafunzi kutembea umbali mrefu wa zaidi ya kilometa sita kufika shuleni.

Mratibu wa elimu shule za msingi kata ya Emboret Bw.Kastul Benedict amesema hali ya elimu katika kata hiyo siyo ya kuridhisha kutokana na wanafunzi kushindwa kufanya vizuri kitaaluma kutokana na uwepo wa changamoto za utoro,upungufu wa walimu pamoja na muamko mdogo wa wanachi wa jamii ya kimasai kusomesha watoto wa kike.

Baadhi ya wananchi wa jamii ya kimasai katika kata ya Emboret wanaiomba serikali kuboresha shule  zilizopo katika maeneo ya wafugaji ili ziweze kutoa elimu bora kwa kuwa wananchi wa jamii hiyo wengi wao wamehamasisika kupelejka watoto wao shule.

Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.

Share habari hii na wenzio wajue

Post a Comment

CodeNirvana
Powered by Blogger.
© Copyright Tazama Line
Back To Top