Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

FREEMAN MBOWE AFUNGUKA NA KUSEMA HAYA JUU YA LOWASSA

Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.
Hatimaye ameingia Chadema. Ilianza kama uvumi lakini jana ilikuwa dhahiri baada ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kutangaza rasmi kukihama chama tawala, CCM na kujiunga na Ukawa kupitia Chadema, huku akisisitiza; “Sasa basi, imetosha.”
Baada ya kukabidhiwa kadi ya Chadema na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, Lowassa alisema amejiunga na chama hicho kikuu cha upinzani ili kutekeleza azma yake ya kuwakomboa Watanzania na kuendeleza safari ya matumaini kupitia Ukawa.
“CCM kimepotoka, kimepoteza mwelekeo na sifa za kuendelea kuiongoza Tanzania,” alisema Lowassa katika mkutano wa kumkaribisha Chadema uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Ledger Bahari Beach na kurushwa moja kwa moja na vituo kadhaa vya televisheni na redio.
Dakika chache baada ya mkutano huo, CCM kupitia mitandao yake ya kijamii ilitangaza kuitisha mkutano wa wanahabari leo mchana kutoa taarifa muhimu, ikiaminika kuwa utakuwa wa kumjibu kiongozi huyo.
Katika mkutano huo, Lowassa alitumia dakika 13 kueleza sababu za kujiunga Chadema, mbele ya wenyeviti wenza wa vyama vinavyounda Ukawa; Mbowe, Dk Emmanuel Makaidi (NLD), James Mbatia (NCCR-Mageuzi) na Prof. Ibrahim Lipumba (CUF).
Katika mkutano huo, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, Naibu wake (Bara), John Mnyika, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu hawakuonekana na hawakupatikana kuzungumzia sababu za kutokuwapo katika tukio hilo muhimu.
Lowassa ambaye aliingia katika ukumbi huo saa 10.20 jioni akiwa ameambatana na mkewe, Regina, watoto wake, ndugu na jamaa, pia aligusia sakata la kampuni ya kufua umeme ya Richmond lililosababisha ajiuzulu wadhifa wa waziri mkuu mwaka 2008, kwamba alifanya hivyo kwa manufaa ya nchi na alishindwa kuvunja mkataba huo kutokana na amri kutoka mamlaka ya juu.
Wakati Lowassa akizungumza, wanachama wa Chadema walikuwa wakiitikia ‘peoples power’, na alipomaliza hotuba yake wanachama wao waliimba wimbo maalumu kuwa wana imani naye, “Tuna imani na Lowaasaa, oya oya oyaa.”
Katika hotuba yake, Lowassa aligusia jinsi mchakato wa kumpata mgombea urais wa CCM ulivyogubikwa na mizengwe na kusisitiza: “Nimetumia muda huu kutafakari kwa kina yaliyotokea Dodoma na hatima yangu katika siasa nchini. Pamoja na yaliyotokea Dodoma azma yangu iko palepale ya kuanza mchakamchaka wa maendeleo ya kuiondoa nchi katika umaskini.
“Najua sote tumevunjika moyo kwa yaliyotokea Dodoma na mazingira yaliyopelekea matokeo yale. Mchakato uligubikwa na mizengwe, ukiukwaji wa maadili, uvunjaji wa katiba na taratibu za uchaguzi za CCM.”
“Sikutendewa haki. Kwa mantiki hii nitakuwa mnafiki kama nitaendelea kujidanganya mimi mwenyewe na umma wa Watanzania kwa kusema kuwa bado nina imani na CCM…,
MWANANCHI
Siku moja baada ya tovuti ya Mwananchi kunukuu habari zilizoripotiwa na Mtandao wa African Review, kuhusu mishahara ya marais wa Afrika na kwingineko duniani, Ikulu imekanusha habari hizo ikisema si za kweli.
Bila kutaja mshahara wa rais ni kiasi gani, taarifa ya Ikulu iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu juzi, ilisema habari hizi siyo za kweli. Ni uongo na uzandiki. Ni uzushi mtupu na ni uzushi wa hatari.
Taarifa ya Ikulu imeikariri ripoti hiyo ya Mtandao wa African Review ikisema: “Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete anashikilia nafasi ya tano miongoni mwa viongozi 38 wa Afrika wanaolipwa mshahara mnono zaidi.
“… Kuwa Rais Kikwete analipwa Dola za Marekani 192,000 kwa mwaka, ikiwa ni malipo ya Dola za Marekani 16,000 kwa mwezi… Mshahara wa Rais kwa mwezi ama kwa mwaka haufikii na hata wala kukaribia kabisa kiwango kinachotajwa na Gazeti la Mwananchi,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo bila kutaja kiwango anacholipwa.
Taarifa hiyo iliendelea kusema: “Tangu Uhuru, mwaka 1961, Rais wa Tanganyika na baadaye tangu mwaka 1964 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekuwa miongoni mwa viongozi wanaolipwa mishahara ya chini kabisa duniani. Mshahara wa Rais wa Tanzania kwa mwezi ni wa chini kiasi cha kwamba mshahara wake unazidiwa, tena kwa mbali na mishahara wanayolipwa baadhi ya watendaji wakuu wa baadhi ya taasisi za umma nchini.
“Ni jambo la kushangaza kwamba Gazeti la Mwananchi, linalochapishwa hapa nchini, linaweza kupata kiasi cha uongo anacholipwa Rais wa Tanzania katika mitandao ya nje badala ya kuuliza rasmi na kupewa majibu sahihi kwa kujiingiza katika uzushi wa kupindua kiasi hiki.
“Gazeti la Mwananchi haliwezi kuwa na nia nyingine yoyote isipokuwa nia ya kuwachochea wananchi na kuwajengea chuki dhidi ya Serikali yao na kiongozi wao mkuu,” ilisema taarifa hiyo ya Ikulu.
Ilimaliza taarifa hiyo kwa kusema: “Ni matarajio yetu, kuwa Gazeti la Mwananchi litafanya jitihada za makusudi, kama taaluma ya uandishi wa habari inavyoelekeza, kutafuta usahihi wa jambo hili na kuwaambia Watanzania ukweli.”

HABARILEO
Taasis ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Singida inamhoji Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba kuhusiana na tuhuma za kukiuka Sheria ya gharama za Uchaguzi na Sheria za Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini.
Hatua hiyo imekuja siku chache tu baada ya wagombea ubunge watatu kati ya wanne wanaogombea jimbo la Iramba, mkoani hapa kugomea mchakato wa kampeni kuelekea kura za maoni wakidai baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Siasa walikuwa wakimbeba mgombea mwenzao, Mwigulu Nchemba.
Wagombea waliogomea zoezi hilo ni Juma Killimbah, David Jairo na Amon Gyunda ambao walisema waliamua kuchukua hatua hiyo kutokana na msimamizi wa uchaguzi kura za maoni CCM katika jimbo hilo, Mathias Shidagisha na msaidizi wake, Mwita Raphael, kubariki wao kuchezewa rafu na Nchemba.
Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Singida Joshua Msuya alisema kuwa Nchemba anahojiwa kutokana na madai ya kukiuka makatazo mbalimbali yaliyoainishwa kwenye Sheria za Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007.
Alisema kuwa makatazo hayo yanajumuisha vitendo vyote vinavyokiuka sheria hiyo kabla ya kampeni, wakati wa kampeni na baada ya kampeni ambapo baada ya uchunguzi wa kutosha kukamilika jalada husika hupelekwa kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU kwa uamuzi wa mwisho.
Kutokana na malalamiko mbalimbali kuifikia ofisi ya TAKUKURU, Msuya ametoa tahadhari kwa wagombea wote wa udiwani na ubunge mkoani hapa kutojihusisha na vitendo vyovyote vinavyoashiria kushawishi wanachama kuwachagua vinginevyo wakigundulika hatua kali dhidi yao zitachukuliwa.
Wakati kampeni zinaendelea kwenye majimbo mbalimbali mkoani hapa, vitendo vya ukiukwaji wa Sheria ya gharama za Uchaguzi vimekuwa vikiripotiwa kwa wingi kuliko wakati mwingine wowote wa kipindi cha uchaguzi.
Aidha, inaripotiwa kuwa hali si shwari katika jimbo la Mkalama kutokana na baadhi ya wagombea wenye uwezo kifedha kudaiwa kumwaga fedha na zawadi mbalimbali kwa wanachama na wananchi wa kawaida ili wagombea hao waweze kuwachagua siku ya kura za maoni itakapofika.
MWANANCHI
Hayawi hayawi sasa yamekuwa. Waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa ameweka rekodi ya kuwa kada wa kwanza aliyewahi kushika nafasi ya waziri mkuu kukihama chama tawala, CCM na kujiunga na upinzani.
Katika orodha ya mawaziri wakuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu uhuru, Lowassa ni waziri mkuu wa tisa kushika madaraka hayo. Alishika wadhifa huo kuanzia Desemba 30, 2005 hadi Februari 7, 2008.
Makada wengine wa CCM waliowahi kushika wadhifa wa waziri mkuu ni, Julius Nyerere, Rashidi Kawawa, Edward Sokoine, Cleopa  Msuya, Dk Salim Ahmed Salim, Joseph Warioba, John Malecela, Frederick Sumaye na Mizengo Pinda.
Lowassa ni kati ya mawaziri watatu waliowahi kuwania urais mara mbili na kushindwa. Wengine ni Malecela (1995 na 2005), Sumaye (2005 na 2015). Mbunge huyo wa Monduli aliyejitokeza 1995 na 2015 na ambaye amekuwa akisononeka namna mchakato wa kupata mgombea ulivyoendeshwa, ameamua kuhamia upinzani ili kuweka haki ndoto ya safari yake ya matumaini.
Katika kipindi cha wiki tatu sasa, kumekuwapo minong’ono ndani na nje ya CCM na kwenye mitandao ya kijamii, kwamba nchi itatikisika kutokana na fununu za Lowassa kuhamia upinzani.
Kulikuwapo kila aina ya propaganda za kubeza hatua hiyo na nyingine zikipongeza na kutahadharisha kuwa, kama angehamia upinzani, ungekuwa mwisho wa CCM.
Tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa, mawaziri wakuu sita wamewahi kuomba kuteuliwa na CCM kupeperusha bendera ya urais na kushindwa, lakini hakuna aliyethubutu kuhama chama hicho tawala.
Mwaka huu, Lowassa alijitosa kwa mara ya pili kuwania urais, akiungana na makada wengine 37 wa CCM waliorudisha fomu wakiwamo Sumaye na Pinda.
Majina ya Lowassa na mawaziri wakuu wenzake hayakupenya hata Tano Bora, yaliishia katika Kamati ya Maadili. Wajumbe watatu wa Kamati Kuu walifichua kile walichodai ukiukwaji mkubwa wa kanuni kwani kamati iliyopaswa kuchuja majina ni Kamati Kuu na siyo Kamati ya Maadili.
Dk Emanuel Nchimbi ambaye amekuwa mjumbe wa CC kwa miaka 17, Sophia Simba na Adam Kimbisa, walitangaza rasmi kujiweka kando na maamuzi hayo ya Kamati Kuu.
HABARILEO
Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, imewataka wafanyabiashara waliojenga vibanda vyao katika eneo la Jangwani, kuvibomoa vibanda hivyo mara moja kabla ya kesho kwa kuwa wamekiuka utaratibu kwa kujenga eneo hatarishi.
Aidha Manispaa hiyo imesema endapo muda waliotoa ukifika agizo hilo likiwa halijatekelezwa watapitisha tingatinga eneo hilo kwa ajili ya kubomoa vibanda hivyo na kisha kuwachukulia hatua wahusika kwa kufanya uvamizi.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi alisema lengo lao lilikuwa ni kuwasaidia wafanyabiashara wanaopanga bidhaa zao barabarani lakini sasa wapo watu waliovamia eneo hilo na kujenga vibanda.
“Tunatangazia wavamizi hao wabomoe mara moja na baada ya hapo kama agizo halitatekelezwa tutabomoa na tutawashitaki kwa uvamizi… Naomba muelewe kwamba Manispaa ya Ilala haijatoa eneo la kujengwa.”
“Ardhi yote iliyopo Manispaa inasimamiwa na Manispaa lakini hakuna mtu aliyejenga katika eneo la Jangwani aliyepewa kibali na Manispaa… Nia ilikuwa kuwasaidia wafanyabiashara wanaotandika bidhaa zao chini ila kwa sasa waliopo pale si wahusika bali ni wavamizi kwa kuwa wanaotandika bidhaa hadi leo wapo mitaani.”
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Isaya Mngurumi alisema walishatamka kwamba eneo hilo haliruhusiwi kujengwa kibanda na waligawa kwa wale wanaotembeza vitu mkononi ili wafanye kama gulio kwa kupanga bidhaa zao chini.
“Lile ni eneo hatarishi kwa ajili ya ujenzi wa kudumu, hivyo likitumika kama gulio kwa kumwaga bidhaa chini, kipindi cha mvua watasitisha biashara lakini waliojenga hawakufuata utaratibu na tunawataka wabomoe mara moja,” alisema.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.

Share habari hii na wenzio wajue

Post a Comment

CodeNirvana
Powered by Blogger.
© Copyright Tazama Line
Back To Top