Inawezekana ukawa ni mmoja kati ya wale ambao wamekua wakijiuliza juu ya utata wa post za Diamond Platnumz ambazo amekua akipost kama zinamhusu mtu au kikundi Fulani ambacho anataka ujumbe huo uwafikie.
Jibu la ‘Caption’ hizo ni hili ambalo Diamond Platnumz analijibu ‘Unajua mimi nimekulia Tandale ni Mswahili kabisa halisi,Uswahili wangu ndiyo naamini umenifikisha hapa,tangu naanza Kamwambie hata ukisikiliza nyimbo zangu zina maneno ya Kiswahili’
Sentensi nyingine ya Diamond amesema>>’hata post zangu ziko Kiswahili
mimi nimejiwekea tu furaha kuwaburudisha watu,mtu asiichukulie tofauti
labda kama mtu ana makusudio yake yeye mabaya,Najua mimi nikirusha jiwe
kwenye giza mtu akilia inamaana limempata inamaana lilikua linamhusu
yeye kama kuna mtu anajishuku basi litakua linamhusu yeye lakini mimi
simlengi mtu yoyote’.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Post a Comment