Rais Jakaya Kikwete
ameliagiza Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, kuanzisha mara moja
mfumo wa ulipaji faini kwa njia ya Benki na mitandao ya simu za mkononi
ili kupunguza ushawishi wa vitendo vya rushwa kwa askari wa kikosi cha
usalama barabarani nchini.
Pia, ameagiza kuanzishwa mfumo wa kuweka
alama kwenye leseni za madereva wanaokiuka sheria na kutumia njia hiyo
kuwafungia, ikiwa ni hatua mojawapo ya kudhibiti wimbi la ajali za
barabarani hapa nchini.
Rais Kikwete alitoa agizo hilo jana
katika viwanja vya Tangamano wakati alipokuwa akizindua Wiki ya Nenda
kwa Usalama Barabarani Kitaifa, inayofanyika mkoani Tanga, ikiwa imebeba
kaulimbiu inayosema ‘Endesha Salama, Okoa Maisha’.
Alisema asilimia 56 ya ajali za
barabarani, zinatokana na uzembe na ukosefu wa umakini kwa madereva na
kwamba hatua hiyo inasababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali na
hata kuathiri ustawi wa Kaya na Uchumi wa Taifa.
“Hivi
mpaka sasa Baraza na Kikosi cha usalama barabarani wanashindwaje
kutumia mifumo ya kidigitali kwa nini mpaka leo hakuna kamera
barabarani? Kwanza ingesaidia kudhibiti ajali na uvunjaji wa sheria,
lakini hata vitendo vya rushwa ambavyo navyo vinachangia ongezeko hili
la wimbi wa ajali hapa nchini,” Rais Kikwete.
Alisema katika kipindi cha miaka mitano
kuanzia mwaka 2010 hadi 2014, jumla ya watu 19,264 walipoteza maisha
kutokana na ajali za barabarani na kwamba idadi ya ya waliokufa katika
kipindi cha mwaka peke yake ni watu 3,534 sawa na idadi ya wanaopeteza
maisha kutokana na ugonjwa wa malaria.
Kufuatia hatua hiyo, amelitaka baraza
hilo kufanya mapendekezo ya marekebisho ya sheria za usalama barabarani
hasa pale penye mapungufu ili kuweza kusaidia kudhibiti wimbi la ajali
linalochangia upotevu wa nguvu kazi ya Taifa.
“Kikosi
cha usalama barabarani kiongeze kasi ya kudhibiti ajali za barabarani
na kuwachukulia hatua za kisheria Askari wanaojihusisha na vitendo vya
rushwa….lakini lisilale katika kutoa elimu ya sheria za usalama
barabarani hasa kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari,” alisisitiza Rais Kikwete.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Post a Comment