Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

RAISI KIKWETE ATAKA FAINI ZOTE ZA BARABARANI ZILIPIWE BANK

Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.
Rais Jakaya Kikwete ameliagiza Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, kuanzisha mara moja mfumo wa ulipaji faini kwa njia ya Benki na mitandao ya simu za mkononi ili kupunguza ushawishi wa vitendo vya rushwa kwa askari wa kikosi cha usalama barabarani nchini.

Pia, ameagiza kuanzishwa mfumo wa kuweka alama kwenye leseni za madereva wanaokiuka sheria na kutumia njia hiyo kuwafungia, ikiwa ni hatua mojawapo ya kudhibiti wimbi la ajali za barabarani hapa nchini.

Rais Kikwete alitoa agizo hilo jana katika viwanja vya Tangamano wakati alipokuwa akizindua Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani Kitaifa, inayofanyika mkoani Tanga, ikiwa imebeba kaulimbiu inayosema ‘Endesha Salama, Okoa Maisha’.

Alisema asilimia 56 ya ajali za barabarani, zinatokana na uzembe na ukosefu wa umakini kwa madereva na kwamba hatua hiyo inasababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali na hata kuathiri ustawi wa Kaya na Uchumi wa Taifa.


“Hivi mpaka sasa Baraza na Kikosi cha usalama barabarani wanashindwaje kutumia mifumo ya kidigitali kwa nini mpaka leo hakuna kamera barabarani? Kwanza ingesaidia kudhibiti ajali na uvunjaji wa sheria, lakini hata vitendo vya rushwa ambavyo navyo vinachangia ongezeko hili la wimbi wa ajali hapa nchini,” Rais Kikwete.

Alisema katika kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2010 hadi 2014, jumla ya watu 19,264 walipoteza maisha kutokana na ajali za barabarani na kwamba idadi ya ya waliokufa katika kipindi cha mwaka peke yake ni watu 3,534 sawa na idadi ya wanaopeteza maisha kutokana na ugonjwa wa malaria.

Kufuatia hatua hiyo, amelitaka baraza hilo kufanya mapendekezo ya marekebisho ya sheria za usalama barabarani hasa pale penye mapungufu ili kuweza kusaidia kudhibiti wimbi la ajali linalochangia upotevu wa nguvu kazi ya Taifa.

“Kikosi cha usalama barabarani kiongeze kasi ya kudhibiti ajali za barabarani na kuwachukulia hatua za kisheria Askari wanaojihusisha na vitendo vya rushwa….lakini lisilale katika kutoa elimu ya sheria za usalama barabarani hasa kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari,” alisisitiza Rais Kikwete.

Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.

Share habari hii na wenzio wajue

Post a Comment

CodeNirvana
Powered by Blogger.
© Copyright Tazama Line
Back To Top