Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

KAMPEINI YA UZAZI WA MPANGO KWA WAKAZI WA KIGOMA KAENI TAYARI

Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika sekta ya afya, wanatarajia kuendesha kampeni ya uhamasishaji wa uzazi wa mpango kwa jamii katika maeneo ya mabaa na vilabu vya pombe mkoani Kigoma.

Meneja Mawasiliano wa Shirika la World Lung Foundation, Victoria Marijani alisema hayo katika mahojiano na waandishi wa habari wakati wa kikao cha wadau kujadili njia mbalimbali za kuwa na mpango wa pamoja na kuendesha kampeni za uzazi wa mpango mkoani Kigoma.

Alisema mkakati huo, unalenga kufikia malengo ya kitaifa ya asilimia 60 ya matumizi ya njia za uzazi wa mpango ili kuongeza uelewa kwa wananchi ambao wakati mwingine hawafikiwi katika kampeni zinazofanyika.

Hata hivyo, Meneja huyo wa World Lung Foundation, alisema umekuwa na mafanikio kiasi katika matumizi ya njia za uzazi wa mpango tangu kuanza kwa kampeni zinazoendeshwa na shirika hilo na watu wameanza kujitokeza katika kutumia njia hizo za uzazi wa mpango.


Mganga Mkuu wa mkoa Kigoma, Dk Leonard Subi alisema bado kuna uelewa wa chini kwa wananchi wa mkoa huo katika kujua elimu ya afya ya uzazi na matumizi ya njia za uzazi wa mpango, ambapo kwa sasa asilimia 14 ya wananchi wa mkoa huo ndiyo wanaotumia njia hizo.

Sambamba na hilo, Dk Subi alisema dini, mila na desturi pia ni kikwazo kwa wananchi katika kutumia njia za uzazi, ambapo wananchi wengi wanaamini kwamba kila mtoto anakuja na riziki yake aliyoandikiwa na Mungu.

Alisema kufanyika kwa mkutano huo wa pamoja wa wadau wanaotoa huduma za afya katika sekta hiyo, kutasaidia kuzifanya kampeni hizo kuwa na mafanikio na kuongezeka kwa uelewa kwa wananchi katika kutumia njia za uzazi wa mpango.

Dk Wilfred Mongo kutoka shirika la EngenderHealth, alisema kuwa bado hakuna wataalamu wa kutosha wa kutoa elimu kwa jamii kuhusu matumizi ya njia za uzazi wa mpango na kwamba kilichopo sasa ni watu wengi kutoa habari kuhusu jambo hilo kuliko kutoa elimu.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.

Share habari hii na wenzio wajue

Post a Comment

CodeNirvana
Powered by Blogger.
© Copyright Tazama Line
Back To Top