Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

KURA ZA MAONI KWA CHAMA CHA MAPINDUZI ZIMEFANYIKA KWA UTULIVU

Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.
Kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), zimefanyika kwa utulivu katika maeneo mengi nchini, huku baadhi ya maeneo kukiibuka hitilafu zilizosababisha baadhi ya wanachama kulala mahabusu.

Mbali na kura hizo za ndani ya CCM zilizopigwa jana nchi nzima, ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kutokuwepo kwa mmoja wa wagombea wa ubunge katika jimbo jipya la Kibamba, kumesababisha chama hicho kuahirisha uchaguzi.

Mkoani Arusha Katibu wa CCM Kata ya Mjini Kati jijini Arusha, Ally Meku na Katibu wa tawi wa CCM katika kata hiyo, Yakub Shamban wametiwa mbaroni na Polisi, baada ya kukutwa na karatasi za kupigia kura za ubunge na udiwani nyumbani wakipiga tiki.

Meku na mwenzake walitiwa mabaroni majira ya saa sita mchana wakati kazi ya kupiga kura ikiendelea katika ukumbi wa CCM Mkoa, kutokana na ofisi ya kata hiyo kuungua kwa moto siku chache zilizopita.


Akithibitisha kukamatwa kwa makada hao, Katibu wa CCM Wilaya ya Arusha, Feruz Banno alikiri kukamatwa kwa wanachama hao na kuongeza kuwa alikwenda Kituo Kikuu cha Polisi kupata taarifa lakini ilishindikana kuwawekea dhamana.

“Ni kweli wametiwa mbaroni na Polisi tangu saa sita mchana… nimefika Kituo cha Polisi na nitafuatilia dhamana zao baada ya uchaguzi ndani ya chama kumalizika,”  Banno.

Alipoulizwa kwa nini katibu huyo alipeleka karatasi nusu kituoni na nyingine kubakiza nyumbani kwake, alisema amefanya kosa kwa kukiuka taratibu za uchaguzi na maelekezo aliyopewa kwa kuwa walikubaliana kila kitu kifanyike hadharani.

Akizungumzia tukio hilo kwa njia ya simu yake ya kiganjani, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, alisema hana taarifa rasmi kwa kuwa yupo nje ya ofisi.
Mkoani Mbeya hali ilikuwa shwari isipokuwa kasoro chache zilizojitokeza kwenye baadhi ya maeneo.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.

Share habari hii na wenzio wajue

Post a Comment

CodeNirvana
Powered by Blogger.
© Copyright Tazama Line
Back To Top