Mchoraji maarufu katika Mji wa Namanyere wilayani Nkasi, Gilbert Paul,
ambaye alishaanza kujiandalia maziko kwa zaidi ya miaka 15 sasa akiwa
hai buheri wa afya, anatarajia kuanza kujichimbia kaburi miezi mitatu
ijayo, ili liwe tayari kuhifadhi mwili wake mara mauti yatakapomfika.
Kijana huyo ambaye amekuwa gumzo mjini
Namanyere na kwingineko, amedai alianza kujiandalia maziko yake kwa
kujichongea msalaba mkubwa na kuusimika juu ya paa la kibanda chake
kilichopo katika Mtaa wa Sasala mjini Namanyere.
Msalaba huo mweupe mkubwa umeandikwa
tarehe aliyozaliwa Desemba 24, 1977 lakini kufa ameweka alama ya ulizo,
huku baadhi ya wageni wanaotembelea mtaa huo wakidhani ni nyumba ya
ibada na wengine wakifikiri ni kaburi la mtu mashuhuri.
“Wageni
wanapoona msalaba huu kwa mara ya kwanza ukiwa umesimikwa juu ya
kibanda hicho, hudhani kuwa ni kaburi kubwa alimozikwa mtu maarufu au
mtawala maarufu wa kimila, kwani kipo katikati kabisa ya mji huu,“ alisema Jackson Nkwabi mkazi wa mjini humo.
Nkwabi alisema msalaba uliopakwa rangi
nyeupe kwa maandishi meusi, umekuwa kivutio cha aina yake kwa wageni
wanaofika mjini hapo ambao ni mara yao ya kwanza kuuona.
Akizungumza na na juzi mjini
Namanyere, Paul alisisitiza kuwa msalaba huo ndio utakaosimikwa katika
kaburi lake ambalo anatarajia kuanza kulichimba Oktoba mwaka huu.
Alisema yuko katika harakati za
kukusanya fedha anazodai kutoka kwa wasitiri wake, ili ifikapo Oktoba
mwaka huu, aanze maandalizi ya kuchimba kaburi ambalo atazikwa mauti
yatakapomkuta.
“Ningekuwa
nimekaribia kuchimba na kusakafia kaburi langu hilo lakini
kinachonikwamisha ni baadhi ya wateja niliowafanyia kazi… nawadai
hawajanilipa wameniahidi kunilipa baadaye mwezi huu wa Agosti,” alisema.
Hii kazi ya uchimbaji wa kaburi
nitaianza Oktoba mwaka huu, ikiwa ni pamoja na kusakafia na kuwekea
nakshi…kaburi langu natarajia ligharimu si chini ya Sh milioni moja
kisha nitatengeneza jeneza litakalo gharimu zaidi ya Sh milioni moja,”
alisema.
Akizungumzia msalaba huo, aliousimika
kwenye kibanda chake cha kazi, Paul alisema aliutengeneza mwenyewe kwa
gharama ya Sh 40,000.
Paul aliyehitimu kidato cha nne katika
Shule ya Sekondari Nkasi mjini Namanyere mwaka 2001, ameoa mke,
Paschalia Salvatory (26) na wamejaliwa mtoto wa kike.
Baadhi ya wakazi wa mjini humo na
kwingineko wanaamini kuwa Paulo anafahamu siku atakayofikwa na umauti,
huku wengine wakimwona amechanganyikiwa, lakini mwenyewe akidai kuwa na
akili timamu na kwamba hajui lini atafikwa na mauti na kwamba anaamini
ataishi miaka mingi ijayo.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Post a Comment