Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

UPORAJI WA SILAHA KWENYE VITUO VYA POLISI UNAUMDHOOFISHA IGP

Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.
Matukio ya uvamizi wa vituo vya polisi yanayokwenda sambamba na kupora silaha, kuua askari na kujeruhi imebainika kuwa yanasukwa na baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu waliopo ndani ya Jeshi la Polisi au waliofukuzwa kwa makosa mbalimbali ukiwa ni mkakati wa kumdhoofisha kiutendaji Mkuu wa Jeshi hilo IGP, Ernest Mangu.

Uchunguzi wa kina umebaini kuwa hatua ya baadhi ya askari polisi kuasi ndani ya jeshi hilo kunatokana na kuchukizwa na mambo kadhaa yaliyofanywa na IGP Mangu tangu alipoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kushika wadhifa huo.

Baadhi ya watumishi wa serikali waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti walisema mambo ambayo yamechukizwa baadhi ya watu ndani ya jeshi hilo ni kutokana na kufukuzwa kazi  askari wengi na wengine kubadilishwa vituo vyao vya kazi kwa sababu mbalimbali, mambo ambayo yamefanyika kipindi cha IGP Mangu.

“Unakumbuka wakati Sanya (Laurance Sanya) alipokuwa RPC Mbeya kulitokea tukio moja la uvamizi wa Kituo cha Polisi Tunduma lakini kipindi cha utawala wa IGP Mangu yamejitokeza mengi hapa kuna sababu,” alisema.

Alisema IGP Mangu amekuwa mkuu wa Jeshi la Polisi ambaye ameongoza kufukuza askari hususani wanaokula rushwa ambao hakuwavumilia na ndiyo hao hao wamegeuka kuwa adui wa jeshi hilo kwa kushirikiana na jamaa na ndugu zao ambao bado wapo ndani ya utumishi wa jeshi hilo.

Jambo la pili lililojenga hasira kwa askari hao ni hatua ya IGP Mangu kutoa tishio kwamba askari wote ambao wana vyeti vya kughushi wajisalimishe.

“Taarifa za Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) inaonyesha kuwa zaidi ya watumishi 10,000 wa Jeshi la Polisi wana vyeti vya kughushi lakini kwa bahati mbaya katika awamu zote za utawala wahusika wamekuwa wakiachwa bila kuchukuliwa hatua na sasa IGP Mangu amekuja kuyavumbua,” kilisema chanzo kutoka ndani ya serikali.


Chanzo hicho kilieleza kuwa baada ya IGP Mangu kutoa tamko la kutaka watumishi ndani ya jeshi hilo wenye vyeti vya kughushi wajisalimishe ndipo matukio ya uvamizi wa vituo vya polisi yalipoibuka kwa kasi ili mkuu huyo wa Jeshi la Polisi aonekane ameshindwa kazi na kufukuzwa.

Anaeleza kuwa kuhusisha matukio ya uvamizi huo na suala la ugaidi inaweza kuwa siyo kweli kwa asilimia kubwa kwa sababu mara nyingi magaidi wanaofanya matukio makubwa mfano nchi jirani wanakuwa na silaha kubwa kama AK-47 sasa inawezekanaje kama kweli ni magaidi hapa kwetu wawe wanapora bunduki ndogo za SMG.

Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Hellen Kijobisimba, alisema matukio ya uvamizi wa vituo vya polisi yameanza kujitengeneza pole pole na sasa yamekuwa makubwa.

Alisema wakati hali ya kiuslama ikibadilika, Jeshi la Polisi kwa upande wake bado halijabadilika ili kukabiliana na matukio hayo.
Zamani usingeweza kuona askari anayetembea barabara ananyang’anywa silaha hata kama huyo askari yukoje, lakini hivi sasa polisi wapo kwenye doria  wanavamia na kunyanng’anywa silaha, wanaenda kama vile nyumbani kwao na bahati mbaya polisi wenyewe hawajashtuka,” alisema.

Kijobisimba alisema polisi wangekuwa wamebadilika kiutendaji matukio hayo  yasingetokea. Alisema sababu nyingine ya kuibuka kwa matukio hayo ni ndani ya Jeshi la Polisi lenyewe kuna tatizo ambalo inabidi litafutiwe ufumbuzi.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.

Share habari hii na wenzio wajue

Post a Comment

CodeNirvana
Powered by Blogger.
© Copyright Tazama Line
Back To Top