Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

KODI ZISIZONA MANUFAA KUFUTWA ASEMA LOWASSA

Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.
Mgombea wa nafasi ya urais kwa tiketi ya Chadema anayeungwa mkono na vyama vinne vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA, Edward Lowassa amesema kama atachaguliwa atahakikisha anafuta kodi ambazo zimekuwa mzigo kwa wananchi wa kipato cha chini.

Wakati upepo wa kisiasa ukizidi kubadilika na huku kadi namba 8 ya CCM ikiwa tayari imekwisha kurejeshwa Dar es Salaam, Mgombea wa urais wa Edward Lowassa anasema kama watanzania watampatia ridhaa ya kuwa rais wa nchi atahakikisha kila mtanzania ananufaika na keki ya taifa akianzia na wafanaykazi wa kada ya chini.
 
Uwepo wa kodi mizigo kwa watanzania wanyonge ni tatizo ambalo serikali yake italishughulikia ndani ya siku 100 za kwanza ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma za jamii hasa katika vituo vya kutolea huduma za afya.
 
Akihutubia maelf ya wakazi mjini hanang ambapo amekuwa mbunge kwa zaidi ya miaka 20, Fredrick Sumaye amewataka wanahanang na watanzania kwa ujumla kutokuhadaika na ahadi butu za CCM, kwani uongozi huo wa CCM ndio umechochea umasikini uliokithiri kwa watanzania.
 
Huku akitumia usafiri wa chopa amefanikiwa kuhutubia mikutano katika maeneo ya Dogobeshi, Magugu, kabla ya kuhitimisha kwa kuhutubia maelf ya wakazi wa jimbo la Hanang mkoan Manyara katika uwanja wa makondeko.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.

Share habari hii na wenzio wajue

Post a Comment

CodeNirvana
Powered by Blogger.
© Copyright Tazama Line
Back To Top