Maendeleo ya kweli na yenye tija kwa wengi yanaanzia kwako wewe binafsi, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya picha hii.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema mshindi wa kiti cha urais atatangazwa rasmi siku ya Alhamisi ambayo ndio leo na kesho yake, atakabidhiwa cheti tayari kwa kuanza shughuli zake.
“Tunatarajia Mungu akijalia, siku ya tarehe 29, saa tatu asubuhi, tutatangaza nani mshindi wa kiti cha rais, na tarehe thelathini tutamkabidhi cheti chake aendelee na shughuli zake,” alisema Mkurugenzi wa Uchaguzi, Kailima Kombwey.
Aidha, tume hiyo imesema haina ‘mbeleko’ ya kumbeba mgombea yeyote, bali itatangaza matokeo kama yatakavyokuwa kwenye masanduku ya kura.
“tume hatuna mbeleko…hatuna mbeleko ya kubeba mtu… Tutatangaza matokeo kama yatakavyokuwa. Koleo tutaita koleo, kisu tutaita kisu.” alisema Kombwey
Mkurugenzi wa Uchaguzi, Kailima Kombwey alisema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya masuala mbalimbali yaliyojiri katika uchaguzi mkuu uliofanyika jana. Kailima alisema uchaguzi umekwenda vizuri.
Alieleza kuwa matokeo ya awali, yataanza kutolewa leo asubuhi na yatakuwa yanatolewa kwa awamu tatu au nne kwa siku kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 12 jioni.
Kombwey alisisitiza kuwa watatangaza ushindi wa kiti cha udiwani, ubunge na urais kulingana na idadi ya kura zilizoko kwenye masanduku ya kura.
Mbali na hayo, Mkurugenzi huyo wa uchaguzi alipongeza kile alichokiita ukomavu mkubwa wa Watanzania, walioonesha kwenye uchaguzi huu ukafanyika kwa amani.
Alisema pamoja na kwamba tume ilijiandaa vyema, pia Watanzania wameonesha ukomavu, kiasi cha uchaguzi kutofautiana na wa mwaka 2005 na 2010 ambao zilishuhudiwa vurugu.
Siku zote bahati yako iko mikononi mwako tu, ili kudhibitisha kuwa ni kweli bofya kwenye picha iliyopo hapa chini.
Never let a problem become an excuse. Put your Problem in Proper Perspective. What is the secret ingredient of tough people that enables them to succeed? Why do they survive the tough times when others are overcome by them? Why do they win when others lose? Why do they soar when others sink? The answer is very simple. It's all in how they perceive their problems.
Share habari hii na wenzio wajue
Post a Comment